Idara ya utabiri wa hali anga imeeleza kuwa baadhi ya sehemu nyingi humu nchini zitashuhudia mvua katika siku chache zijazo.

Ripoti  iliyotolewa na idara hiyo ya hali ya anga inaonyesha kuwa mvua itashuhudiwa katika maeneo ya nyanda za mashariki ya juu na magharibi mwa bonde la ufa, kusini na kati ya bonde la ufa pamoja na ziwa victoria.

Vilevile baadhi ya sehemu za pwani na kaskazini mashariki pia zitashuhudia mvua kubwa huku baadhi ya maeneo katika kaunti za Turkana na Marsabit zikishuhudia upepo mkali.

March 14, 2023