Mahakama Kuu jijini Nairobi imeamuru kwamba akaunti za kibinafsi za benki zilizosajiliwa kwa majina ya Msajili Mkuu wa Idara ya Mahakama, Anne Atieno Amadi, pamoja na mwanawe Brian Ochieng Amadi na wengine wawili zizuiliwe.

Hii ni baada ya Bi Amadi kushtakiwa pamoja na mwanawe Brian na kampuni ya Dubai inayohusika na dhahabu.

Katika ombi hilo, Bruton Gold Trading LLC inadai kuwa washukiwa, kwa niaba ya kampuni ya uwakili ya Amadi and Associates Advocates, walipata kinyume cha sheria zaidi ya Ksh.89 milioni kwa dhahabu ambayo hawakuwahi kutoa.

Kampuni hiyo inadai kuwa ilikuwa na nia ya kununua dhahabu kutoka Kenya na ilitambulishwa na mmoja wa washukiwa hao, Daniel Ndegwa Kangara.

Walidai kuwa baada ya makubaliano kati ya pande hizo, Kangara alikuwa apeleke dhahabu ambayo ingesafirishwa kwenda Dubai kuuzwa.

Walalamishi hao wanadai kuwa uchunguzi wa DCI ulibaini kuwa Amadi ndiye wa akaunti ambayo pesa hizo ziliwekwa. Zaidi ya hayo, wanadai kuwa fedha zilizopokelewa na kampuni hiyo zilitolewa taslimu na mtoto wa Bi Amadi na watu wengine wawili bila nyaraka za kutosha kama inavyotakiwa na Sheria ya Mapato ya Uhalifu na Kupambana na Utakatishaji wa Pesa.

Katika karatasi za mahakama, kampuni ya Dubai inadai kuwa Bi Amadi baadaye aliwapigia simu akitaka kufuta kiasi hicho ndani ya miezi sita, ambapo walikataa kwa vile hakukuwa na utendakazi wa usalama kwa upande wa washtakiwa.

May 19, 2023