Waziri wa elimu Ezekiel Machogu amebuni upya baraza la mtaala wa mtihani katika vyuo vya kiufundi humu nchini.

Kwa mujibu wa Machogu ni kwamba baraza hilo litathmini ubora wa elimu na mitihani katika vyuo hivyo.

Aidha amelitaka baraza hilo jipya kutoa mafunzo yanayofikia viwango vya kimataifa ili kuwandaa wanafunzi kusaka ajira katika mataifa ya kigeni kama vile Ujerumani ambalo lina mahitaji ya wafanyakazi wenye ujuzi wa taaluma za kiufundi.

June 27, 2023