BY ISAYA BURUGU 19TH AUG 2023-Rais William Ruto amefanya  mazungumzo na Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir katika Ikulu ya Nairobihivi leo .Rais Ruto amesema Kenya imejitolea kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili na Sudan Kusini kwa manufaa ya raia wa mataifa hayo mawili.

Rais alisema nchi hizo mbili zinafuata miradi ya pamoja ya miundombinu ili kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kukuza biashara. Kenya, ameongeza, ina nia ya kutekeleza miradi ya miundomsingi chini ya mradi wa Lamu Port-Sudan Kusini-Ethiopia-Transport Corridor (LAPSSET).

Hii, alielezea, itaongeza muunganisho, ushirikiano zaidi na kukuza biashara ya ndani ya kanda kwa ustawi wa pamoja.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

August 19, 2023