Mtandao wa kijamii unaotumia video fupi kupitisha maudhui wa Tiktok utafanya kazi na Kenya katika mchakato wa kutekeleza mageuzi na kufuatilia maswala yanayochapishwa na wakenya katika mtandao huo.
Hatua hiyo ,kwa mjibu wa rais Wiliam Ruto itahakikisha kuwa yanayochapishwa kwenye jukwaa hilo na wakenya yanafuata miongozo iliyokubaliwa.
Rais Ruto kwenye mkutano wa njia ya video na mkurugenzi mkuu wa Tiktok Shou Zi Chew wamekubaliana kuwa watahakikisha yanayochapishwa kwenye mtandao huo yanafaa kwa kila mwanajamii.
Hatua hiyo inamaanisha kuwa iwapo mmoja atachapisha maswala yasiyofaa katika mtandao huo yataweza kuondolewa mara moja.
Wakati wa mkutano huo Chew pia alikubali kuanzisha afisi ya Tikotok humu nchini ili kusaidia katika kutekeleza oparesheni zake katika bara la Afrika.Ameahidi kuwaajiri wakenya Zaidi kufanya kazi katika jukwa hilo.
𝐓𝐈𝐊 𝐓𝐎𝐊 𝐓𝐎 𝐌𝐎𝐃𝐄𝐑𝐀𝐓𝐄 𝐈𝐓𝐒 𝐂𝐎𝐍𝐓𝐄𝐍𝐓
Short-form video hosting service TikTok will work with Kenya in reviewing and monitoring its content.
The move, President @WilliamsRuto said, will ensure that content on the platform adheres to agreed guidelines.
In a… pic.twitter.com/6vYh4xxWHe
— State House Kenya (@StateHouseKenya) August 24, 2023