Waziri wa ulinzi Aden Duale hii leo amezindua hazina ya operesheni za Amani itakayoiwezesha serikali kuwatuma wanajeshi kwenye oparesheni za Amani nchini na kimataifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo katika kambi ya kahawa Garrison, Duale amesema kuwa hazina hiyo pia itawawezesha wanajeshi wa KDF kupokea mafunzo ili kujisawazisha na wanajeshi wengine katika ngazi za kimataifa.Kando na hayo, hazina hiyo itawasaidia kujiami kwa magari na silaha.

February 1, 2024