Naibu wa Rais Rigathi Gachagua ameahidi kuwa wakenya hawatakua na haja ya kuhofu kuhusu kufurushwa makwao kiholela au kubomolewa makaazi yao nyakati za usiku.
Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa shule ya Komarok jijini Nairobi alikoandamana na Rais William Ruto, Gachagua amesema kwamba serikali ya Rais William Ruto imetoa ilani kwa viongozi wote watakaotekeleza maagizo yoyote ya kuwafurusha wananchi kutoka kwa makaazi yao pasi na kujadiliana na idara za usalama katika kaunti husika. Naibu wa rais amesisitiza wakenya watakao furushwa kutoka katika ardhi ambayo si yao watapata maeneo mbadala watakapoishi.
SAUTI: Kauli ya Naibu wa Rais Rigathi Gachagua
Katika hafla hiyo aidha, Rais William Ruto aliahidi kuwa wizara ya ardhi imeanzisha juhudi za kutoa zaidi ya hatimiliki 4000 za shamba kwa wakaazi katika kaunti ya Nairobi, kama mojawapo ya njia za kukabiliana na matatizo yanayoibuka kuhusu ardhi katika kaunti hiyo pamoja na kutoa nafasi kwa wananchi kutekeleza miradi ya maendeleo bila hofu.
Soma Pia
- Aliyekuwa Seneta wa Kakamega Cleophas Malala aachiliwa huru. April 10, 2025
- TAHADHARI YA MAFURIKO: Waziri Ngeno Awataka Wakazi wa Narok Kuwa Macho April 9, 2025
- Baadhi ya wakaazi wa Narok walalamikia kutofanya kazi kwa SHA. April 7, 2025
- Narok Yajiandaa Kumkaribisha Rais Ruto kwa Ziara ya Maendeleo ya Siku Mbili April 7, 2025
- Mawaziri Wateule Ruku na Cheptumo Kupigwa Msasa na Bunge Aprili 14 April 4, 2025