BILL GATES AWASILI KENYA

BY ISAYA BURUGU 1TH NOV,2022-Tajiri  wa Marekani Bill Gates yuko humu nchini ambapo amepangiwa  kufanya msururu wa mazungumzo ya umma.Mwanzilishi huyo wa Microsoft anatazamiwa kukutana na maafisa wa serikali na washikadau wengine katika sekta ya kibinafsi.Gates atazuru kaunti ya Makueni ambako atakaribishwa…

Kithure Kindiki

Waziri wa usalama atoa onyo kali kwa wahalifu Jijini Nairobi.

Waziri wa usalama wa ndani Prof Kithure Kindiki ametoa Onyo kali kwa wahalifu wanaowahangaisha wananchi katika maeneo tofauti ya taifa, akisema kuwa serkali imeweka mipango kabambe ya kukabiliana nao ili kuhakikisha kuwa wakenya wanaendelea kutekeleza majukumu yao kwa amani pasi na hofu…

Idara ya polisi iko ngangari kukabiliana na visa vya uhalifu.

Inspekta jenerali wa polisi Japheth Koome amesema kuwa idara ya polisi iko ngangari kukabiliana na visa vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikishuhudiwa katika miji mbalimbali. Kwenye kikao na waandishi wa habari, Koome amedokeza kuwa watatumia njia zote walizo nazo kushughulikia wizi kwa kutumia…

Wakenya wahimizwa kutokuwa na hofu kufuatia wimbi la saba la ugonjwa wa korona. .

Kaimu mkurugenzi mkuu katika wizara ya afya dkt. Patrick Amoth amewahimiza wakenya kutokuwa na hofu kufuatia wimbi la saba la ugonjwa wa korona unaoshuhudiwa humu nchini. Akizungumza na waandishi wa habari, Amoth amesema kuwa hakuna haja ya kurejesha vizuizi vya kukinga ugonjwa…

Kenta aondoa kesi ya kupinga kuchaguliwa kwa Patrick Ntutu kama gavana wa Narok

BY ISAYA BURUGU ,14TH NOV,2022-Aliyekuwa mwaniaji wa ugavana kaunti ya Narok kupitia tikiti ya ODM Moitalel Ole Kenta, mapema hii leo aliwasilisha ombi la kutaka kuondoa kesi ya kupinga ushindi wa gavana wa sasa Patrick Ntutu.Mbunge huyo wa zamani wa Narok Kaskazini…

Mwili wa mtoto wa miezi sita wapatikana umetupwa chooni Narok

 BY ISAYA BURUGU ,14TH ,NOV,2022-Mwili wa mtoto wa miezi 9 umepatikana ukiwa umetupwa chooni katika mtaa wa total viungani mwa mji wa narok.Haya ni kwa mujibu wa mzee wa mtaa huo wa total jacob jomo ambaye amesema kwamba alipata taarifa hiyo kutoka…

Wanabodaboda wahimizwa kujiunga na vyama vya ushirika ili kupunguza uhalifu.

Wanabodaboda chini ya muungano wa Eminent jijini Nairobi, hii leo wamefanya mkutano na wakuu wa polisi kutoka eneo hilo kufuatia ongezeko la visa vya uhalifu vinavyodaiwa kutekelezwa na waendesha bodaboda. Akizungumza wakati wa mkutano huo, kamanda wa oparesheni katika kituo cha polisi…

Kikosi cha kwanza cha wanajeshi wa KDF chaelekea nchini DRC.

Mkuu wa Majeshi Robert Kibochi amewataka wanajeshi wa kenya kushirikiana vyema na wenzao wakati ambapo wanaelekea nchini DR Congo kwa oparesheni ya kulinda amani nchini humo. Hatua hiyo inajiri wiki moja baada ya Rais William Ruto kuamuru kutumwa kwa wanajeshi 900 kutoka…