Maafisa nane wa kitengo cha SSU kuzuiliwa kwa siku 21 zaidi.

Maafisa nane kati ya tisa wa kitengo cha SSU kilichovunjwa wamerudishwa rumande huku mmoja wao akiachiliwa kwa dhamana ya kima cha shilingi laki tano. Tisa hao walifikishwa katika mahakama ya kahawa mbele ya hakimu Diana Mochache ambapo mmoja wao aliweza kudhibitisha kuwa…

KCCB yawapongeza wakenya kwa kudumisha amani.

Baraza la maaskofu wa kanisa katoliki KCCB, limewapongeza wakenya kwa kudumisha amani, wakati na baada ya uchaguzi mkuu ulioandaliwa tarehe tisa mwezi agosti mwaka huu. Wakitoa taarifa kwa vyombo vya habari, baraza hilo limewahimiza viongozi waliochaguliwa kuweka kando masuala ya siasa na…

Uwanja wa ndege wa Bukoba nchini Tanzania wafunguliwa tena kufuatia ajali ya ndege iliyogharimu maisha ya abiria 19

BY ISAYA BURUGU/BBC,10,NOV 2022-Uwanja wa ndege wa Bukoba kaskazini – magharibi mwa Tanzania umefunguliwa tena kufuatia ajali iliyosababisha vifo vya watu 19. Ndege hiyo ya abiria ilianguka katika Ziwa Viktoria ilipokuwa ikijaribu kutua kwenye uwanja huo Jumapili iliyopita.Afisa utawala katika mji huo…

Wahudumu wa Bodaboda Kisii waanzisha mikakati ya kujilinda dhidi yahalifu

BY ISAYA BURUGU 10 NOV,20222-Wahudumu wa bodaboda mjini Kisii wamezindua mikakati ya kujihakikishia usalama.Hatua hiyo inafuatia kuongezeka kwa visa vya uhalifu vinavyowahusu wahudumu hao. Inaripotiwa kuwa wahalifu wamekuwa wakiwaendea wahudumu hao kwenye stendi wakijifanya abiria na wanapobebwa wakifika njiani wanageuka na kuwavamia…

Mshukiwa wa wizi wa Ng’ombe auawa na umati Transmara Kusini kaunti ya Narok

BY  ISAYA BURUGU,10,NOV 2022-Mtu mmoja ameaga dunia baada ya kupigwa na umma akifumaniwa kuiba Ng,ombe eneo la Trasmara kusini. Akithibitisha kisa hicho naibu kamishana wa Trasmara kusini George Onyango amesema Jamaa huyo ameuawa katika kaunti jirani ya Migori eneo la Kehanja  katika…

Gideon Moi

Gideon Moi ajiondoa kwenye kinyang’anyiro cha kuelekea EALA.

Kinara wa Chama cha Kanu Gideon Moi amejiondoa katika kinyang’anyiro cha kuwania wadhifa wa kuliwakilisha taifa katika bunge la Afrika Mashariki (EALA) Kwa mujibu wa Taarifa ya Katibu wa maswala ya kisiasa katika chama cha KANU Fredrick Okango seneta huyo wa zamani…

Japheth Koome

Japheth Koome aidhinishwa kuwa Inspekta Jenerali wa Polisi nchini.

Koome ambaye alikua kamanda wa polisi katika chuo kikuu cha mafunzo ya polisi cha Kiganjo, aliteuliwa kutwaa wadhifa huo baada ya mtangulizi wake Hillary Mutyambai kuchukua likizo ya muda mrefu kutokana na matatizo ya kiafya.

Mahakama kutoa uamuzi iwapo itaondoa kesi inayomkabili Naibu Rais Gachagua.

Mahakama inatarajiwa kutoa uamuzi kuhusu iwapo itaondoa kesi ya ulaghai inayomkabili Naibu Rais Rigathi Gachagua na watu wengine tisa. Hii ni baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha ombi la kutaka kesi hiyo iondolewe kwa misingi kuwa uchunguzi wa kesi hiyo haujakamilika.Kwa mujibu…