NACADA yatarajia kupokea fedha zaidi ili kupambana na pombe haramu na mihadarati.

Waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki ametangaza kuwa Mamlaka ya Kitaifa ya Kampeni Dhidi ya Matumizi Mabaya ya Pombe na dawa za Kulevya NACADA itaongezewa fedha ili kuiwezesha kupambana na kero la unywaji wa pombe na matumizi ya dawa za kulevya…

VIDEO: Mswada wa Fedha upo wazi kwa Marekebisho – Mbunge Ndindi Nyoro awaeleza Wakenya.

Ndindi Nyoro, amesema kwamba mswada wa fedha bado uko wazi kwa marekebisho zaidi ili kuhakikisha kwamba sauti ya wananchi inapata nafasi kwenye mswada huo.

Musalia Mudavadi awataka wakenya kujitolea katika kulipa ushuru.

Hakuna taifa linaloweza kupiga hatua za maendeleo bila kuwa na mfumo unaofaa wa kukusanya ushuru. Haya ni kwa mujibu wa waziri mwandamizi nchini Musalia Mudavadi, ambaye amewasuta wanaokosoa mapendekezo yaliyo katika mswada wa fedha wa 2023/24  akiwataka kutoa mapendekezo mbadala ya jinsi…

Serikali kujenga shule tano maalum chini ya Mpango wa Amani katika kaunti ya pokot magharibi.

Waziri wa usalama wa ndani na Utawala wa Kitaifa Kithure Kindiki ametangaza kuwa serikali itajenga shule tano maalum chini ya Mpango wa Amani. Shule hizo tano Dira, Todo, Tuwit, Lomuke, na Chepchoren, zitahakikisha wanafunzi kutoka Kaunti za Elgeyo Marakwet, Baringo na Pokot…

Spika Wetangula

Vuta nikuvute bungeni Spika Wetangula akisita kuidhinisha kutimuliwa kwa Sabina Chege.

Shughuli za kawaida katika bunge la taifa alasiri ya leo, zilisitishwa baada ya kizaazaa kuibuka kuhusiana na uamuzi wa kumbandua Sabina chege kama naibu mnadhimu wa walio wachache katika bunge hilo. Katika uamuzi wake, spika Wetangula alieleza bunge kwamba agizo la mahakama…

Raila Odinga ametoa matakwa kwa Rais William Ruto kuhusu Mswada wa Fedha wa 2023.

Kiongozi wa Azimio la umoja Raila Odinga ametoa matakwa kumi kwa Rais William Ruto kuhusu Mswada wa Fedha wa 2023. Raila sasa anamtaka Ruto akome kuwalemea Wakenya na badala yake azingatie kupunguza gharama ya maisha. Akizungumza jijini Nairobi Raila pia amemtaka Ruto…

Waziri Kindiki aagiza kukamatwa kwa viongozi walihusika na uhasama eneo la Trans Mara.

Waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki ametoa agizo la kutiwa nguvuni kwa viongozi wote waliohusika katika vurugu zilizoshuhudiwa katika mpaka wa maeneo ya Nkaararo na Enoreteet huko Trans Mara, Kaunti ya Narok. Akizungumza Siku ya Jumatao ya leo katika kaunti ya…

Kamishna Isaac Masinde azuru mpaka wa Nkararo na Enoreteet huku mzozo ukiendelea.

Kamishna wa kaunti hii ya Narok Isaac Masinde amezuru mpaka wa Nkararo na Enoreteet kule Transmara ambapo mzozo umekuwa ukiendelea kwa siku nne mfululizo. Mzozo huo umesababisha uharibifu wa mali huku nyumba kadhaa zikiteketezwa. Jamii za Isiria na irwasingishu zimekuwa zikizozania mpaka…