BY ISAYA BURUGU,15TH MARCH,2023-Tume ya maadili na kukabiliana ufisadi EACC  imewaonya  wahasibu wa kaunti   kuhusu matumizi yasiyofaa ya mfumo wa ulipaji fedha.Kwenye notisi kutoka kwa afisa mkuu mtendaji wa  tume hiyo Twalib Mbarak  amewaonya mahasibu hao  akiwagiza kuhakikisha kuwa  mifumo bora  itakayohakikisha  kuwepo kwa uwazi  katika ulipaji  wa fedha umewekwa kikamilifu.

Mfumo wenye dosari unahusu malipo ya mapema wanayopewa wafanyikazi mbali mbali na maafisa wa kaunti  ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao rasmi.Baadhi ya vitendo vya ukiukaji maadili vilivyogunduliwa Katika kuteleza malipo hayo ni  ulipaji fedha kwa njia ya mikono bila kutumia mfumo hitajika au kuwepo mifumo miwili ya ulipaji fedha hizo kwa wakati mmoja.

EACC inasema baadhi ya maafisa huidhinisha malipo hayo kwa niaba ya wenzao ,huku maombi ya fedha hizo yakihidhinishwa bila kufuata utaratibu unaohitajika.

March 15, 2023