BY ISAYA BURUGU 23RD OCT,2023-Kiongozi wa chama cha Narc-Kenya Martha Karua na Katibu Mkuu wa Chama cha Jubilee Jeremiah Kioni hivi leo wamezindua  rasmi Kongamano la Uongozi la Kamwene, mungano  ambao wanasema utakuwa wa kukuza masilahi kutoka eneo la Mlima Kenya.

Akiwahutubia wanahabari jijini Nairobi, Karua amesema bado ni wanachama dhabiti wa muungano wa Azimio La Umoja One Kenya – ambapo yeye ni mkuu mwenza – licha ya uvumi kuwa vazi hilo jipya lilikuwa likiashiria kuwepo kwa mpasuko ndani ya upinzani ulipotangazwa kwa mara ya kwanza mwezi Septemba.

Alipuuza maoni ya kiongozi wa Azimio Raila Odinga aliyoyatoa Jumapili iliyopita (na baadaye yakafafanuliwa kuwa alinukuliwa vibaya) ambayo yalionekana kuwa ni uidhinishaji rasmi wa kiongozi wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka kama mpeperushaji bendera wa upinzani katika uchaguzi mkuu wa 2027.

Alipoulizwa kuhusu maoni yake kuhusu kisa ambapo Odinga alimuunga mkono Musyoka katika uchaguzi wa 2027, kiongozi huyo wa Narc-Kenya alipuuzilia mbali mazungumzo kama vile ya kukatisha tamaa.

 

 

October 23, 2023