BY ISAYA BURUGU,3RD OCT,2023-Mashirika ya kiserikali  yameagizwa kupunguza matumizi yao kwa asilimia 10 katika mwaka huu wa fedha ili kuwianisha matumizi yao na rasilimali zilizopo.

Rais William Ruto alitoa maagizo hayo kama sehemu ya hatua za kubana matumizi ili kuhakikisha mashirika ya serikali yanakabiliana na msukosuko wa uchumi duniani.

Hatua hiyo inalenga kupunguza kiwango cha matumizi ya kifedha katika utumishi wa umma na kuiondoa nchi kutoka kwa mzigo wa deni la umma.Rais alitoa onyo kwa maafisa wa serikali wanaotaka kukwepa matumizi ya mfumo wa malipo wa umoja, akisisitiza ulazima wa uangalizi bora.

Shinikizo zimekuwa zikiongezeka kwa serikali ya Kenya kupunguza gharama ya juu ya maisha inayochochewa na kupanda kwa bei ya vyakula na mafuta.

Hii ni kwa sababu kuongezeka kwa kodi kutawalemea walipa kodi ambao mapato yao yanayoweza kutumika yameathiriwa na gharama ya juu ya maisha huku kwa upande mwingine upunguzaji wa matumizi ukileta ukuaji zaidi wa pato.

Serikali ya Kenya Kwanza Alliance inafuatilia mchakato wa uimarishaji wa fedha, ikiwa ni pamoja na kuweka kifuniko kwa ukopaji mpya kama sehemu ya hatua za kuanzisha ufufuaji wa uchumi unaolegalega kutokana na kupanda kwa mfumuko wa bei, uhaba wa dola ya Marekani na kupungua kwa akiba ya fedha

October 3, 2023