Naibu wa Rais Rigathi Gachagua ameahidi kuwa wakenya hawatakua na haja ya kuhofu kuhusu kufurushwa makwao kiholela au kubomolewa makaazi yao nyakati za usiku.
Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa shule ya Komarok jijini Nairobi alikoandamana na Rais William Ruto, Gachagua amesema kwamba serikali ya Rais William Ruto imetoa ilani kwa viongozi wote watakaotekeleza maagizo yoyote ya kuwafurusha wananchi kutoka kwa makaazi yao pasi na kujadiliana na idara za usalama katika kaunti husika. Naibu wa rais amesisitiza wakenya watakao furushwa kutoka katika ardhi ambayo si yao watapata maeneo mbadala watakapoishi.
SAUTI: Kauli ya Naibu wa Rais Rigathi Gachagua
Katika hafla hiyo aidha, Rais William Ruto aliahidi kuwa wizara ya ardhi imeanzisha juhudi za kutoa zaidi ya hatimiliki 4000 za shamba kwa wakaazi katika kaunti ya Nairobi, kama mojawapo ya njia za kukabiliana na matatizo yanayoibuka kuhusu ardhi katika kaunti hiyo pamoja na kutoa nafasi kwa wananchi kutekeleza miradi ya maendeleo bila hofu.
Soma Pia
- Marekani Yasitisha Ufadhili wa Umoja wa Mataifa kwa Operesheni Haiti. February 5, 2025
- SUSWA | Mafisa wa Polisi Wapewa Makataa ya Siku Tano Kuhama Eneo Hilo. January 30, 2025
- Wanachama wa kamati ya kuwateua makamishna wa IEBC waapishwa. January 27, 2025
- Zoezi la kuchanja mifugo kote nchini kuzinduliwa wiki ijayo. January 22, 2025
- Magavana Wataka Kufutwa kwa Agizo la Kusitisha Utoaji wa Basari za Wanafunzi January 21, 2025