Mvua kubwa inatarajiwa kuendelea kunyesha katika maeneo mengi ya nchi, kulingana na utabiri wa kila wiki wa Idara ya Hali ya Hewa nchini. Kulingana na mtaalamu wa hali ya hewa, dhoruba huenda zikatokea katika baadhi ya maeneo ya Nyanda za Juu Mashariki na Magharibi mwa Bonde la Ufa, nyanda za chini za Kusini-mashariki, Pwani na Kaskazini-mashariki mwa nchi.

Mvua za asubuhi za mara kwa mara pamoja na mvua za alasiri na usiku na ngurumo za radi zinatarajiwa katika kaunti za Siaya, Kisumu, Homabay, Migori, Kisii, Nyamira, Trans Nzoia, Baringo, Uasin Gishu, Elgeyo-Marakwet, Nandi, Nakuru, Narok, Kericho, Bomet, Kakamega, Vihiga, Bungoma, Busia na Pokot Magharibi.

November 24, 2023