Mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya nchini NACADA sasa imebaini kwamba dawa za kulevya zinazosababisha watu kupoteza fahamu inayojulikana kama Fentanyl hazijaingia nchini.

Ripoti hii imetolewa wiki mbili baada ya sampuli kuchukuliwa pwani mwa kenya kufuatia video zilizosambazwa zikionyesha vijana waliokuwa wameduwaa na wengine kupoteza fahamu.

Hata hivyo mamlaka hiyo imesema kwamba asilimia kubwa ya vijana wameanza kutumia dawa zilizochanganywa na zile zinazowafanya mifugo kulala wanapofanyiwa matibabu.

September 8, 2023