Raila Odinga

BY ISAYA BURUGU,6TH NOV,2023-Kinara wa Upinzani Raila Odinga hivi leo amesema kuwa Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya hautatia saini mkataba wa pande mbili iwapo suala la gharama ya juu ya maisha halitashughulikiwa.

Akizungumza mjini Mombasa, Odinga alisema Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo, ambayo inaongozwa na Kiongozi wa Bunge la Kitaifa Kimani Ichung’wah na kinara wa Azimio La Umoja Kalonzo Musyoka, lazima pia ikubaliane kuhusu kukaguliwa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Makataa ya miezi mitatu ya kamati kuwasilisha ripoti yake inakaribia kwa kasi Novemba 26.

Wiki ijayo, kamati hiyo inatarajiwa kurudi nyuma ili kuandaa ripoti yake.Hata hivyo, Odinga ameshikilia msimamo thabiti kwamba hakuna mwafaka utakaoafikiwa isipokuwa suala la gharama kubwa za maisha na ukaguzi wa uchaguzi halitashughulikiwa vilivyo.

.

Alikuwa akizungumza mjini Mombasa wakati wa hafla ambapo aliandamana na Gavana wa Mombasa Abdulswamad Nassir kwa ajili ya kukabidhi vifaa vya matibabu katika Hospitali ya Kaunti ya Port Reitz.Odinga alielezea wasiwasi wake kutokana na kuendelea kwa shida zinazowakabili Wakenya.

 

November 6, 2023