Pope Francis amzika Pope Benedict XVI

BY ISAYA BURUGU 3RD AUG 2023-Papa mtakatifu  Francis  amewataka vijana  kutilia maanani utunzaji wa dunia na mabadiliko ya hali ya Anga  akitaja kama kiungo muhimu  kinachohitaji kulindwa  kwa kupigana na umaskini na chagamoto zingine za kijamii.

Papa Francis mwenye umri wa miaka 86 amefanya utunzjai wa mazingira  lengo lake  kupitia  nyayo yake ya  “Laudato Si”  inayo taka kila juhudi kuelekezwa katika utunzaji wa mazingira.

Papa amesema hayo wakati akiwahutubia Zaidi ya wanafuzni  6500 katika chuo kikuu katoliki cha Lisbon katika siku yake ya pili ya ziara yake nchini ureno.

Papa aliwasili mjini Lisbon jana jumatano  kuhudhuria hafla ya siku ya vijana duniani  ambayo ni sherehe  ya wiki moja ya kimataifa ya kikatoliki inayotarajiwa kuwavutia watu milioni moja.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

August 3, 2023