BY ISAYA BURUGU,4TH NOV,2023-Makachero wa DCI kaunti ya Nyeri wamefanikiwa kumtia mbaroni mwanamume wa miaka 32 anayeshukiwa kuwa mwizi wa simu na kunasa simu Zaidi ya 417.

Kulingana na taarifa hiyo iliyochapishwa kwenye kurasa za mitandao ya kijamii ya DCI, Kupatikana na kukamatwa kwake kulifuatia kuhojiwa kwa vijana wawili waliokamatwa awali na maafisa wa upelelezi wa Nyeri, baada ya kuzuiliwa walipokuwa wakipora simu kutoka kwa wanunuzi huko Gatitu, Nyeri.

Vitu vingine vilivyopatikana vimefichwa katika eneo lake la biashara ni pamoja na seti mbili za TV, kompyuta ndogo tatu, kamera mbili, kadi 47 za simu za wateja, kichapishi cha HP miongoni mwa vingine.

Haya yote yalikamatwa na kuwekwa kama ushahidi.

Kamati ya usalama ya Nyeri imeonya dhidi ya ongezeko la wadukuzi ambao wengi wanavutiwa na simu janja, lakini inawahakikishia umma kwamba mashirika yoyote yanayohusika yapo kwenye rada za polisi na hivi karibuni watakabiliwa na nguvu kamili ya sheria.
Wakati huo huo, Mshukiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya jumatatu.

 

 

November 4, 2023