Wakenya wapatao 240,000 katika kaunti ya Narok wanakumbwa na makali ya njaa baada ya kushuhudiwa kwa vipindi virefu vya jua na ukame unaokumba kaunti 23 kote nchini. Ni kutokana na hali hii ambapo viongozi wa serikali ya kaunti ya Narok wakiongozwa na gavana Patric Ole Ntutu pamoja na viongozi wa sekta mbalimbali katika kaunti ya Narok wameanzisha juhudi za kuwasaida wananchi kukabiliana na makali ya njaa. Gavana Ntutu pamoja na kamishena wa Narok Bw.Isaac Masinde wameongoza kikao cha kujadili mbinu mwafaka za kuwasaidia wananchi walio katika hatari zaidi.

Akiwahutubia waandishi wa habari nje ya Ofisi yake kamishena Isaac Masinde amesema zaidi ya shule 130 katika kaunti ya Narok zinahitaji msaada wa chakula kutokana na makali ya njaa. Masinde amesema kuwa serikali kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali wanafanya juhudi  za pamoja ili kuhakikisha kuwa wamesamabaza chakula cha msaada kwa maeneo yaliyoathirika. 

Gavana Ntutukwa upande wake amesema kuwa sehemu zilizokabwa zaidi na njaa ni maeneo ya Mosiro Narok mashariki, Narosura, maji moto, eneo la Loita, Naikara, kapsasian eneo la Ilkeren Trasmara magharibi pamoja na eneobunge la Emurua Dikirr. Ntutu amesema serikali ya kaunti ya Narok itashirikiana na ile ya kitaifa kuhakikisha kuwa misaada mbali mbali imewafikia wakazi wa maeneo haya. 

Taarifa zaidi

Naibu Rais Kithure Kindiki Atoa Wito kwa Viongozi wa Kidini Kuikosoa Serikali kwa Upendo

Naibu Rais Kithure Kindiki amewahimiza viongozi wa kidini nchini kuikosoa serikali kwa njia ya upendo na heshima, akisema…

Kenya Iko Njiani Kudhoofika Kiuchumi Mbunge Ndindi Nyoro Aonya.

Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro, ameonya kuwa Kenya iko kwenye hatari ya kushindwa kulipa madeni yake na kudhoofika…

Kamati ya Bunge Yaidhinisha Uteuzi wa Geoffrey Ruku na Hanna Cheptumo kuwa Mawaziri

Kamati ya uteuzi katika Bunge la Taifa imeidhinisha uteuzi wa mawaziri wateule Geoffrey Ruku na Hanna Cheptumo baada…

October 11, 2022