Serikali ya Kenya imeahirisha mpango wa kufungua tena vituo vya mpaka kati ya Kenya na Somalia.

Akizungumza alipokutana na viongozi wa usalama katika kaunti ya Garissa, waziri wa usalama wa ndani na mipango ya kitaifa Kithure Kindiki alisisitiza kuwa kucheleweshwa huko ni muhimu ili kukabiliana na ongezeko la hivi karibuni la mashambulizi ya kigaidi na uhalifu ambao umekumba eneo la kaskazini mashariki katika miezi ya hivi karibuni.

Serikali inalenga kutoa ulinzi zaidi kwa raia wake huku ikihakikisha uzingatiaji wa majukumu ya kimataifa.Kando na hayo alielezea umuhimu wa kutanguliza usalama wa taifa na kulinda maslahi ya wakimbizi na jamii zinazowahifadhi.

July 5, 2023