UDA

Chama Tawala cha UDA kimetangaza rasmi kuiunga mkono azma ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga katika kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Muungano wa Umoja wa Afrika (AU).

Katibu wa Kitaifa wa UDA, Cleophas Malala, alitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari, akifafanua kwamba uamuzi huo wa chama umetokana na kutambua mchango wa Raila Odinga katika kuwa mstari wa mbele katika kukuza demokrasia na maendeleo barani Afrika.

Malala alisisitiza kwamba hatua ya UDA kumuunga mkono Raila Odinga haina lengo la kisiasa, bali inatokana na kutambua juhudi zake za kuleta mabadiliko chanya katika bara la Afrika. UDA imeeleza kuwa inaamini kwamba uongozi wa Odinga unaweza kuwa na athari chanya katika kufanikisha malengo ya Muungano wa Umoja wa Afrika, kuhimiza maendeleo endelevu, na kukuza demokrasia katika nchi za Kiafrika.

Kauli yake imeungwa mkono na mnadhimu wa Wengi wa Bunge la Kitaifa, Silvanus Osoro, ambaye ameeleza kwamba chama hicho kitafanya mkutano wa  wajumbe wa kitaifa ili kujadili uungaji mkono wa Raila kugombea uenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika.

 

February 17, 2024