Vatican imetangaza mazishi ya Papa yatafanyika Jumamosi, Aprili 26 kuanzia saa 10:00 asubuhi.Papa Francis atapelekwa kwenye Basilica ya St Peter siku ya Jumatano asubuhi saa 09:00.
Jeneza la Papa liatasalia katika basilibca ya St. Peter’s hadi siku ya mazishi ilikuwapa waumini fursa kutoa heshima zao za mwisho.Mwili wake kwa sasa umewekwa kwenye jeneza katika kanisa la makazi ya Santa Marta, ambapo aliishi wakati wa upapa wake wa miaka 12.
Vatican ilikuwa imetangaza hapo awali kwamba Papa Francis alifariki kutokana na kiharusi.Papa alifariki Jumatatu ya Pasaka, Aprili 21, 2025.
Mkurugenzi wa idara ya Afya na Usafi wa Jimbo la Vatican, Andrea Arcangeli alitoa cheti rasmi cha kiini cha kifo cha Papa. Mazishi ya Papa Francis yatafanyika nje, mbele ya Kanisa kuu la Mtakatifu Petro.
Mkuu wa Chuo cha Makardinali, Giovanni Battista Re, ataongoza ibada hiyo.
The body of the late Pope Francis will be transferred to St. Peter’s Basilica on Wednesday at 9:00 AM to lie in state until his funeral on Saturday morning at 10:00 AM.
The Holy See Press Office announced on Tuesday that Cardinal Giovanni Battista Re, Dean of the College of… pic.twitter.com/ObGjYl7Bi7
— Vatican News (@VaticanNews) April 22, 2025