KINDIKI KITHURE - Radio Osotua

BY ISAYA BURUGU,9TH NOV,2023-Waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki amesema kuwa mpango wa serikali kuwatuma wanajeshi wapatao 1000 kulinda amani nchini Haiti hautadhiri usalama wa taiafa hili.

Akizungumza bungeni hivi leo,Waziri amesema cha muhimu ni kuhakikisha kuwa maafisa wa polisi wa humu nchini wanapewa mafunzo bora kutekeleza kazi zao hillo linatosha.

Ameendelea kusema kuwa kilicho muhimu ni utekelezaji bora wa majukumu ya polisi.

Waziri amefika bungeni kujibu maswali kutoka kwa wabunge kuhusu mpango wa polisi wa kenya Kwenda Haiti saw ana hali ya usalama ilivyo nchini.Kikao hicho pia kimehudhuriwa na inspekta mkuu wa polisi Japheth Koome.

November 9, 2023